Pages

Home » » Rekodi ya Messi yapingwa, yupo Mzambia aliyewahi kufunga magoli 107.

Rekodi ya Messi yapingwa, yupo Mzambia aliyewahi kufunga magoli 107.


Chama cha Soka cha Zambia (Faz) kimesema kinakusudia kuikabili Fifa ili iweze kuitambua kazi iliyofanywa na mshambuliaji Godfrey Chitalu wa nchi hiyo kwa kufunga magoli 107 mwaka 1972.

Hatua hiyo imefuatia Lionel Messi kutangazwa kuvunja rekodi ya Mjerumani Gerd Mueller ya kufunga magoli 85, ambapo kwa sasa mwanasoka huyo wa Argentina ana magoli 88 kufikia mwaka huu 2012.

Msemaji wa chama cha Soka cha Zambia (Faz) Eric Mwanza amekaririwa akiiambia BBC Michezo kuwa, chama hicho kinazo rekodi za kudhibitisha kazi ya Chitalu, hivyo kutaka mchango wake katika soka utambuliwe kimataifa.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger