Pages

Home » » Wanafunzi 20 wafariki Marekani, Rais Obama amwaga chozi

Wanafunzi 20 wafariki Marekani, Rais Obama amwaga chozi

Rais ObamaRais wa Marekani Barack Obama ameviagiza vyombo vya dola kuwashughuli wale wote waliohusika katika kuishambulia shule ya Msingi ya Connecticut  na kusababisha vifo vya wanafunzi 20.

Akizungumza Ikulu kwa masikitiko makubwa huku akitoa machozi, Rais Obama alisema kitendo cha kuwaua wanafunzo hao ni cha kinyama na hakiwezi kuvumiliwa hivyo ni vema watu wote waliohusika katika shambulio hilo wakakamatwa na kuchukulia hatu kubwa za kisheria.

Uchunguzi wa awali ubebaini kuwa mtu aliyekuwa anafyatua risasi zilizo sababisha vifo hivyo ni Adam Lanza ambaye naye aliweza kufariki katika sakata hilo.

"nimeviagiza vitengo vya usalama kuhakikisha kuwa vinatafuta kila uwezekano wa kuwachukulia hatua wahusika, na kutafuta chanzo cha uvamizi huo, mana haiwezekani mtu aanze kuvamia eneo bila sababu,"alisema Rais Obama.

Taarifa imeeleza kuwa wanafunzi 18 waliweza kufariki papo hapo wakati wengine wawili walikufa wakiwa wanapatiwa huduma ya kwanza hospitalini, pia watu wazima sita nao wamekufa akiwemo mtu mmoja anayedhaniwa kuwa alikuw miongoni mwa wafyatua risasi

Hili ni tukio la pili linalofanana na lile lililotokea mwaka 2007 katika shule ya Virginia Tech.

Rais Obama akielezea masikitiko yake kwa njia ya televisheni huku akipangusa machozi kila mara alisema pamoja nakutokea vitendo hivyo mara kwa mara lakini sasa juhudi zinahitajika ili kukomesha kabisa jambo hilo.

"Ninatoa rambirambi zangu kwa familia zote zilizokumbwa katika mkasa huu, najua mpo katika kipindi cha majonzi makubwa, ila nataka muelewe kuwa pamoja na urais wangu mimi pia ni mzazi, nimejeruhiwa kama jinsi walivyojeruhiwa wazazi wengine wa Amerika,"alisema
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger