Pages

Home » » WANAHABARI WA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI WAENDELEA KUFUNDWA MKOANI RINGA KUHUSU SENSA

WANAHABARI WA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI WAENDELEA KUFUNDWA MKOANI RINGA KUHUSU SENSA

Waandishi wa habari kutoka mkoa wa Mbeya wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma akisoma risala kwa waandishi wa Habari toka katika mikoa ya Nyanda za juu kusini.
Washiriki wasemina waandisho toka mkoa wa Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi baada ya kufungua rasmi mafunzo hayo.

Waandishi toka Mkoa wa Rukwa na Katavi

Wenyeviti wa vilabu vya waandishi wa habari toka mikoa ya nyanda za juu kusini pamoja na lLndi na Mtwara wakiwa katika picha moja na Mgeni rasmi pamoja na viongozi wengine
Mwenyekiti wa IPC Mwangosi akiongea na baadhi ya waandishi waliofika katika semina
Mratibu wa sensa Iringa Fabian Fundi katikati akiwa na wadau wengine katika semiana hiyo

Picha kwa Hisani ya Fransis Godwin


Mkuu wa mkoa wa Iringa Dokta CHRISTINE ISHENGOMA amewataka wanahabari kulisaidia Taifa katika zoezi la sensa ya watu na makazi kwa kuendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza katika zoezi hilo.

Mkuu huyo wa mkoa ametoa Rai hiyo katika ukumbi wa Ruco mjini Iringa wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili ya wanahabari kutoka mikoa ya nyanda za juu kusini pamoja na mkoa wa Lindi na Mtwara.

Alisema kuwa zoezi hilo la sensa ya watu na mkazi lina nafasi kubwa katika Taifa ili kuwezesha kupanga bajeti kulingana na mahitaji sahihi ya wananchi wake.

Aidha amesema kuwa sensa ya watu na makazi ni zoezi ambalo limekuwa likifanyika kila baada ya miaka 10 hivyo lazima umma kujulishwa ili kujitokeza kwa wingi katika zoezi Hilo.

Wakati huohuo amewataka wakuu wa kaya kuweka kumbukumbu sahihi ambazo zitawezeshwa makalani wa sensa kupata taarifa zilizo sahihi katika kufanikisha zoezi Hilo.

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger