Waandishi wa habari kutoka mkoa wa Mbeya wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma akisoma risala kwa waandishi wa Habari toka katika mikoa ya Nyanda za juu kusini.
Washiriki
wasemina waandisho toka mkoa wa Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na
mgeni rasmi baada ya kufungua rasmi mafunzo hayo.

Wenyeviti
wa vilabu vya waandishi wa habari toka mikoa ya nyanda za juu kusini
pamoja na lLndi na Mtwara wakiwa katika picha moja na Mgeni rasmi pamoja
na viongozi wengine
Mwenyekiti wa IPC Mwangosi akiongea na baadhi ya waandishi waliofika katika semina
Mratibu wa sensa Iringa Fabian Fundi katikati akiwa na wadau wengine katika semiana hiyo
Picha kwa Hisani ya Fransis Godwin
Mkuu wa
mkoa wa Iringa Dokta CHRISTINE ISHENGOMA amewataka wanahabari kulisaidia Taifa
katika zoezi la sensa ya watu na makazi kwa kuendelea kuhamasisha wananchi
kujitokeza katika zoezi hilo.
Mkuu huyo
wa mkoa ametoa Rai hiyo katika ukumbi wa Ruco mjini Iringa wakati wa ufunguzi
wa mafunzo ya siku mbili ya wanahabari kutoka mikoa ya nyanda za juu kusini
pamoja na mkoa wa Lindi na Mtwara.
Alisema
kuwa zoezi hilo
la sensa ya watu na mkazi lina nafasi kubwa katika Taifa ili kuwezesha kupanga
bajeti kulingana na mahitaji sahihi ya wananchi wake.
Aidha
amesema kuwa sensa ya watu na makazi ni zoezi ambalo limekuwa likifanyika kila
baada ya miaka 10 hivyo lazima umma kujulishwa ili kujitokeza kwa wingi katika
zoezi Hilo.
Wakati
huohuo amewataka wakuu wa kaya kuweka kumbukumbu sahihi ambazo zitawezeshwa
makalani wa sensa kupata taarifa zilizo sahihi katika kufanikisha zoezi Hilo.

0 comments:
Post a Comment