Mwenyekiti mpya wa Mbeya Press Club aliye simama ndugu Christopher Nyanyembe akitoa Shukrani zake
Ilikuwa
ni mapema baada ya uchaguzi ambapo kiongozi mpya Christopher Nyanyembe
alipongezana na mpinzani wake, kiongozi huyo mpya ameshinda kwa kura 27
Hapa iikuwa ni nderemo na vifijo
Waandishi wa habari wakiwapongeza viongozi wapya
Hii
Ndio kamati kuu Iliyo chaguliwa katika kuendesha Klabu ya waandishi
Mbeya, akiwemo mwandishi mkuu wa Mbeya yetu Ndugu Joseph Mwaisango wa
Kwanza kulia kwa walio simama
Waandishi wa Habari wakijiandaa na mkutano huo wa uchaguzi
Waandishi wa habari wakisikiliza kwa umakini, Wa kwanza kabisa anaitwa Ndugu Mwakipesile
Waandishi wa Habari wakichukuwa yanayojili katika mkutano huo mkuu
Baadhi ya waandishi wa habari wakifurahia Jambo
Mtangazaji wa Bomba FM Dj Fredy Helbert Aliye valia Tshirt nyeusi kati kati akifuatilia kwa umakini mkutano mkuu
Kikao Cha uchaguzi kinaendelea
Na Gabriel Mbwille, Kyela.
Hatimae
mwenyekiti wa chama cha wanahabari mkoa wa Mbeya CHRISTOPHER NYENYEMBE
amefanikiwa kutetea nafasi yake baada ya kumsihinda mpinzani wake mwanahabari
kutoka kituo cha televishion cha Taifa HOSEA CHEYO kwa kura 27 kati ya 49
zilizopigwa.
Uchaguzi
huo umefanyika wilayani Kyela ambapo HOSEA CHEYO alipata kura 22 wakati
NYENYEMBE akipata kura 27, nafasi ya makamu mwenyekiti wa chama hicho
imechukuliwa na MODEST NKULU kwa kupata kura 26 dhidi ya kura alizopata
mpinzani wake MAMA LAWA aliyepata Kura 22.
Nafasi ya
mweka hazina wa klabu imechukuliwa na PENDO FUNDISHA aliyepita bila kupigwa
huku nafasi ya katibu MERALI CHAWE mwandishi wa habari kutoka HABARI LEO
akishindwa kutetea nafasi yake kwa kubwagwa na KENETH MWAZEMBE aliyepata kura
31 dhidi ya 17 alizopata CHAWE.
Aidha
nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na CHARLES MWAKIPESILE kwa kipindi kirefu sasa
imechukuliwa na MESHAKI NJAVIKE, nafasi ya Uchumi, mipango na mafunzo
imechukuliwa na FESTO SIKAGONAMO.
Kwa upande
wa wajumbe ni CHARLES MWAKIPESILE, EASTER MACHA na JOSEPH MWAISANGO.















0 comments:
Post a Comment