Pages

Home » » Rwanda kuwasilisha mashtaka yake kwa Ban Ki moon

Rwanda kuwasilisha mashtaka yake kwa Ban Ki moon

Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda amesema kuwa nchi yake inakusudia kuwasilisha mashtaka yake kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusiana na ripoti ya umoja huo inayodai kuwa Kigali inawasaidia waasi wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Louise Mushikiwabo amesema kuwa, ripoti ya Umoja wa Mataifa inayoituhumu Rwanda kuwa inawaunga mkono waasi wa Kongo ni pungufu.
Ujumbe wa Wataalamu wa Umoja wa Mataifa unazituhumu Rwanda na Uganda kuwa zinawaunga mkono waasi wa Kongo ambao hivi sasa wanadhibiti maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo kubwa ya katikati mwa Afrika.
Kundi hilo la wataalamu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linasema kuwa, licha ya Rwanda na Uganda kukanusha vikali madai hayo lakini hadi hivi sasa zinaendelea kuwaunga mkono waasi wa M23 wanaoendesha mapigano dhidi ya serikali ya Kinshasa hasa katika mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger