Pages

Home » » MBUNGE AHAHIDI KUHAMASISHA MGOMO KWA WANANCHI KATIKA MAENDELEO ENDAPO SERIKALI ITASHINDWA KUTATUA KERO KWA WAFUGAJI JIMBONI KWAKE.

MBUNGE AHAHIDI KUHAMASISHA MGOMO KWA WANANCHI KATIKA MAENDELEO ENDAPO SERIKALI ITASHINDWA KUTATUA KERO KWA WAFUGAJI JIMBONI KWAKE.


Mbunge wa jimbo la Mbozi Magharibi akihutubiwa wananchi wake.
 
Viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi na Momba wametakiwa kuhakikisha wanafuatilia kero ya muda mrefu ya wafugaji wanaoishi pembezoni mwa ziwa Rukwa kutozwa faini pasipo kupewa stakabadhi.

Hayo yalisemwa na mbunge wa jimbo la Mbozi magharibi DEVID SILINDE wakati wa mahojiano na Bomba Fm kuhusu sakata hilo na kuongeza kuwa endapo uongozi wa Serikali hautoweza kulifuatilia suala hilo wananchi watagoma kuchangia fedha hizo ikiwa ni pamoja na fedha nyingine za maendeleo.

Alisema tatizo hili la faini kiholela limekuwa mtaji kwa watu na viongozi wote wa halmashauri na wilaya wamekwisha fikishiwa taarifa kwa ajili ya ufuatiliaji zaidi wa tatizo hilo.

“Kwa sasa tumetoa kipindi hiki cha sikukuu kwa viongozi wa hlamahauri kuhakikisha tatizo hilo wanalimaliza na vinginevyo tutahamaisha wananchi wasishiriki hata kidogo katika shughuli za maendeleo kwani wamekwisha nyonywa vya kutosha.”alisema Silinde

Wakati huohuo alitoa wito kwa wakazi wa wilaya ya Momba kujitokeza kwa wingi katika kuchangia harambee ya kuchangia upatikanaji wa huduma ya maji na elimu ambapo harambee hiyo itahudhuriwa pia na wabunge mbalimbali hapa nchini

“Harambe hiyo imelenga kutafuta ufumbuzi wa tatizo Sugu la maji na elimu katika halmahaur yetu ya mji wa Tunduma na wilaya ya Momba kwa ujumla” alisema Silide.

Kuhusu tatizo la njaa jimboni mwake amesema hatua za haraka zimeanza kuchukuliwa kwa kusambazwa kwa chakula katika kata na kaya zinazokabiliwa na tatizo hilo wanapatiwa chakula

“Hakuna tatizo la njaa kwa wananchi kwa sasa kwani hatua zimeanza kuchukuliwa na hadi sasa tumekwisha gawa mahindi kwa kila kata inayokabiliwa na matatizo hayo ambapo zoezi la usimamizi wa chakula hicho limekabidhiwa kwa madiwani kwani wao ndio wenyeviti wa kata”.



Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger