
Mfanyakazi
wa mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Iringa (IRUWASA)
akiwajibika kuzibua chemba iliyozibwa na kulalamikiwa na wananchi
kupitia mtandao huu wa radio Nuru Fm asubuhi ya leo

Diwani wa kata ya Makorongoni Iringa na wananchi wakishuhudia zoezi la kuzibua chemba iliyoziba

Baada
ya wananchi kuulalamikia ungozi wa mamlaka ya maji safi na maji
taka mjini Iringa (IRUWASA) kwa kushindwa kutimiza wajibu wake kwa
kuzibua chemba zilizozibwa ,wafanyakazi hao wamefika eneo la tukio
asubuhi hii kuzibua chemba hiyo iliyolalamikiwa kwa zaidi ya miezi
mitatu sasa
BAADA YA HALI HIYO DIWANI ATOA MWEZI MMOJA KWA WANANCHI WAKE KUACHA MARA MOJA KUTUPA TAKA OVYO.

Diwani
wa kata ya Makorongoni mjini Iringa Tadeus Tenga akizungumza na
wananchi wake asubuhi hii katika kipindi cha Gari ya matangazo radio
Nuru Fm kinacchoendeshwa kwa ushirikiano na mtandao huu ni kipindi kipya
ambacho kimeanza leo na kitaendelea kila siku saa 2 asubuhi na jioni
saa 11

Hali
ya uchafu katika eneo la mwembetogwa ambapo wananchi wanatupa taka
katika mto mchambawima baada ya kukosa chombo cha kuwekea taka


Chemba
za maji taka kutoka katika vyoo zikiwa zimefumka bila matengenezo
kutoka mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Iringa (IRUWASA)

Diwani Tenga akitoa muda wa mwezi mmoja kwa wananchi wake kuacha kutiririsha maji ovyo


Diwani
wa kata ya Makorongoni mjini Iringa Mhe.Tadeus Tenga ametoa muda wa
mwezi mmoja kwa wananchi wa kata hiyo kuacha kutiririsha maji taka
ovyo huku akiitaka mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Iringa
(IRUWASA) kufanya kazi bila kusukumwa na wananchi .
Diwani
Tenga ametoa kauli hiyo leo katika mahojiano maalum na Jamii yangu.
Amesema kuwa hali ya usafi
katika kata hiyo ni mbaya sana na kuwa kutokana na hali hiyo
amelazimika kutoa muda wa mwezi mmoja kwa wananchi wa kata hiyo
kufanya usafi huku akiijia juu Iruwasa kwa kutaka kutembelea maeneo
mbali mbali badala ya kukaa ofisini.
Diwani huyo amekili kuwa
hali ya ufisa na chemba za maji taka kuziba katika eneo hilo kuwa
ni sugu na hivyo kutaka jitihada za haraka kufanyika ili kuepusha
kipindu pindu
0 comments:
Post a Comment