Pages

Home » » WANANCHI WATEKETEAZA MATREKTA KATIKA SHAMBA LINALOMILIKIWA NA KANISA LA EFATHA HUKO SUMBAWANGA

WANANCHI WATEKETEAZA MATREKTA KATIKA SHAMBA LINALOMILIKIWA NA KANISA LA EFATHA HUKO SUMBAWANGA

 
Matrekta hayo yakiwa yameteketea kabisa kwa kuchomwa moto katika shamba hilo inalomilikiwa na kanisa la Efatha mkoani Rukwa.

(PICHA,  HABARI  NA JOSHUA MWAKABUNGU  SUMBAWANGA)
……………………………………………….
Shamba la Malonje linalomilikiwa na Kanisa la Efatha limepata hasara kubwa baada ya wananchi wa kijiji cha 
Sikaungu wilayani Sumbawanga vijijini mkoani Rukwa, kujichukulia sheria mkononi na kuvamia moja ya kambi ya
Shamba hilo iitwayo Sikaungu na kuyateketeza kabisa matrekta mawili makubwa aina ya New Holland na kubomoa 
baadhi ya nyumba kwenye kambi hiyo.
 
Mchungaji Kiongozi Michael Meela wa Kanisa la Efatha mkoani Rukwa akiongelea kuhusu suala hilo alisema hasara 
iliyopatikana ni zaidi ya shilingi milioni 228 na kwamba tukio hilo lilitokea mara tu baada ya Mbunge wa Jimbo la Kwela
Mh. Ignas Malocha kuhutubia mkutano wa hadahara kijijini hapo na kuwahamasisha wananchi watumie nguvu ya umma 
kuyakomboa mashamba yao yaliyochukuliwa na mwekezaji huyo.
 
Kamnda wa polisi wa mkoa wa Rukwa Bw Jacob Mwaruanda akithibitisha kuhusu sakata hilo alisema tayari wanawashikilia
watu 11 kwa tuhuma za kufanya uharibifu huo mkubwa na kwamba wanatarajiwa kufikishwa wakati wowote mahakamani

 
Matrekta hayo yakiwa yameteketea kabisa kwa kuchomwa moto katika shamba hilo inalomilikiwa na kanisa la Efatha mkoani Rukwa.
 
Moja ya makambi yaliyoteketea kwa kuunguzwa na moto wakati wananchi hao walipovamia mashamba hayo na kuchoma moto zana za kilimo katika shamba hilo.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger