Pages

Home » » FILIKUNJOMBE AMNUSURU SPIKA KWA DENI LA AHADI YA TSH 50,000

FILIKUNJOMBE AMNUSURU SPIKA KWA DENI LA AHADI YA TSH 50,000

 Mbunge  Filikunjombe
                                      Diwani wa kata ya Ruhuhu Edwin Haule Spika


Katika hali isiyotegemewa mbunge  wa  jimbo la Ludewa mkoani Njombe Deo Filikunjombe alilazimika  kumnusuru diwani  wa kata ya Ruhuhu Bw Edwin Haule Spika  kuzomewa na wapiga   kura  wake baada ya  kudaiwa kushindwa  kutimiza ahadi yake ya shilingi 50,000 ambayo  aliitoa wakati  wa kampeni  za uchaguzi mwaka 2010.

Wakizungumza katika mkutano huo kwa jazba mbele ya mbunge  huyo  wananchi wa kata ya Ruhuhu  walisema  kuwa  hawana imani hata kidogo na  diwani  wao  huyo mheshimiwa Spika kutokana na kuwatapeli  kiasi  cha  shilingi 50,000 ambacho aliahidi  wakati  wa kampeni na hivyo kudai  kuwa hawapo tayari  kumsikiliza katika mkutano huo wa mbunge ambao ni kwamara ya kwanza  wanamwona diwani huyo  toka uchaguzi mkuu  wa mwaka2010.

Grece Haule  alisema  kuwa  diwani  huyo aliahidi  fedha hizo kwa ajili ya kuchangia  ujenzi wa Zahanati  ulioanza  toka mwaka 2004 hadi  sasa bila  kukamilika  na kuwa mbali ya  kuwa Halmashauri ni kikwazo cha kukamilika kwa Zanahati  hiyo  ila diwani wao pia anachangia kwa kiasi kurudisha  nyuma maendeleo .

Kutokana na madai  hayo ya  wananchi  mbunge Filikunjombe alilazimika kumsimamisha  diwani huyo ili  kutekeleza ahadi  hiyo ila hakuweza  kuanya   hivyo kutokana na kukosa  kiasi hicho cha  fedha na hivyo kuwaomba wapiga kura  wake  kuendelea  kumvumilia mkopo huo wa ahadi hadi hapo atakapofanikiwa  kupata  fedha.

" Mheshimiwa  mbunge na  wananchi naomba kupewa  muda  nitakaa na  wananchi ili kumaliza  deni hilo ....naomba mnivumilie "


Kutokana na diwani huyo  kushindwa  kulipa  fedha  hizo mbunge  alilazimika  kumlipia fedha hizo kiasi cha shilingi 50,000 na kuwaongeza  kiasi cha shilingi 500,000 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi  wa wodi la mama na mtoto kijijini hapo.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger