Pages

Home » » LICHA YA MKUU WA MKOA WA RUKWA KUTUMIA ZAIDI YA MASAA NANE KUSULUHISHA MGOGORO WA WAUMINI WA KANISA ANGLIKANA JIMBO LA ZIWA RUKWA MJINI SUMBAWANGA SULUHU YASHINDIKANA

LICHA YA MKUU WA MKOA WA RUKWA KUTUMIA ZAIDI YA MASAA NANE KUSULUHISHA MGOGORO WA WAUMINI WA KANISA ANGLIKANA JIMBO LA ZIWA RUKWA MJINI SUMBAWANGA SULUHU YASHINDIKANA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na waumini wa kanisa la Anglikanala watakatifu wote Jimbo la Ziwa Rukwa mjini Sumbawanga jana katika ukumbi wa RDC mjini Sumbawanga katika jitihada zake za kuunganisha dayosisi hiyo baada ya kuwa na mpasuko wa muda mrefu wa zaidi ya miaka miwili wa makundi mawili moja likiwa linatii mamlaka ya kanisa Anglikan kwa kumkubali Askofu Kasagara kama kiongozi wao kanisani aliyesimikwa mwaka jana tarehe 16, Juni kwa mujibu wa katiba ya kanisa hilo na wengine wanaompinga kwa madai kuwa hana sifa za kuwa kiongozi wao na kwamba kwenye uchaguzi uliomchagua alitumia rushwa.
 
Katika kikao kilichodumu kwa zaidi ya masaa nane ikiwa ni dhamira ya Mkuu huyo wa Mkoa kutafuta suluhu ya migogoro yote iliyopo Mkoani Rukwa ukiwepo huu wa kanisa Anglikan muafaka ulishindwa kupatikana kutokana na upande unaompinga askofu kuchelea kutoa maamuzi ya kuteua wajumbe watano watakaoungana na wajumbe wengine watano kutoka upande wa wanaotii mamlaka kushirikiana na Kiongozi huyo wa Mkoa kutafuta suluhu ya mwisho kushindikana na kudai wapewe muda zaidi kutafakari yote yaliyozungumzwa na ndipo wafanye uteuzi wa wajumbe hao.
 
Baada ya ushawishi mkubwa uliotumika Mkuu wa Mkuu wa Rukwa aliona kuwa dhamira halisi ya kumaliza mgogoro huo kwa baadhi ya waumini hususani wanaompinga Askofu haipo na kwamba msimamo wao uko pale pale wa kumpinga kiongozi huyo. Alihitimisha kwa kusema kuwa ataandika taarifa yake na kuifikisha panapostahiki taarifa itakayoonyesha kuwa kundi moja lipo tayari kutoa ushirikiano wa kumaliza mgogoro na lingine linalompinga Askofu Kasagara kutokuwa na utayari wa kutoa ushirikiano unaostahiki. Alimalizia kwa kusema kuwa ataliandikia Kanisa lichukue maamuzi kulingana na taratibu zao za kikanisa. 
 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na waumini wa Kanisa hilo katika ukumbi wa Ofisi ya  Mkuu wa Mkoa wa Rukwa (RDC) jana.
Baadhi ya waumini wa kanisa la Anglikana watakatifu wote Jimbo la Ziwa Rukwa mjini Sumbawanga wakimsikiliza kwa makini Mkuu huyo wa Mkoa aliyekuwa akijaribu kuwaweka sawa juu ya umuhimu wa kuungana na kuacha tofauti zao kwa maendeleo ya kanisa lao na Mkoa kwa ujumla. Baadhi ya waumini hususan wanaompinga Askofu wa kanisa hilo jimbo la Ziwa Rukwa wameweka msimamo wao kuwa hawamtaki kiongozi huyo
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger