Pages

Home » » MKUU WA MKOA WA RUKWA AFUNGA SEMINA ELEKEZI YA SIKU MBILI YA MADIWANI WA CCM MKOANI RUKWA LEO

MKUU WA MKOA WA RUKWA AFUNGA SEMINA ELEKEZI YA SIKU MBILI YA MADIWANI WA CCM MKOANI RUKWA LEO

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na wajumbe wa semina elekezi ya madiwani wa CCM wa Mkoa wa Rukwa wakati akifunga semina hiyo iliyoanza jana na kumalizika leo katika ukumbi wa Manispaa ya Sumbawanga. Kushoto ni Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Rukwa Ndugu Hiporatus Matete. Semina hiyo iliyokuwa ya mafunzo ilikuwa na lengo la kuimarisha utendaji kazi wa chama hicho pamoja na kukiongezea chama uwezo zaidi wa kuisimamia shughuli za Serikali katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wa chama hicho pamoja kukiongezea nguvu zaidi kiweze kushinda katika uchaguzi ujao wa mwaka 2015.
 
Semina hiyo ilikuwa na jumla ya mada tisa amabazo ni historia ya CCM tangu TANU na ASP, Katiba ya CCM ya mwaka 1977-2012, Sera za msingi za CCM, Muelekeo wa Sera za CCM mwaka 2010-2020, Sera za Umma, Utekelezaji wa sera Ya CCM ya Ujamaa na Kujitegemea katika mazingira ya utandawazi na uchumi wa soko, Hali ya kisiasa na mikakati wa ushindi kwa ajili ya uchaguzi Mkuu 2015, Uandishi wa katiba mpya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na Majukumu yatokanayo na taarifa ya kazi na maazimio ya Mkutano Mkuu wa 8 wa CCM 2012.   
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa Ndugu Hiporatus Matete, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya, Muwezeshaji wa Semina hiyo kutoka Sekretarieti ya CCM na Mbunge wa Jimbo la Kalambo CCM Ndugu Josephat Kandege ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Semina hiyo. 
 
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Rukwa Ndugu Hiporatus Matete akizungumza kwenye ufunguzi wa semina hiyo jana. Katika maneno yake ya ufunguzi alisema lengo kuu la semina hiyo ni kuimarisha chama kiweze kushika dola kwa kutatua kero zinazowakabili wananchi wa Mkoa wa Rukwa na taifa kwa ujumla. Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alisema Serikali haiwezi kufanya kazi peke yake bila ya msukumo kutoka katika chama, aliwataka viongozi katika ngazi zote kuwa mstari wa mbele katika kufanya shughuli za maendeleo badala kukaa tu ofisini na kuagiza walio chini yao.
 
Kiongozi wa wakufunzi wa semina hiyo Ndugu Lukasi Kisasi akijitambulisha kwa wajumbe wa semina hiyo.
Baadhi ya madiwani waliohudhuria semina hiyo wakiskiliza kwa makini moja ya mada zilizowasilishwa kwenye semina hiyo, jumla ya madiwani 64 wameshiriki kwenye semina hiyo.
 
Madiwani kutoka kata tofauti za Mkoani Rukwa wakifuatilia semina hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa akizungumza katika Semina hiyo. (Picha na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger