Pages

Home » » Mamlaka ya mapato (TRA) kurasimisha kazi zaTasnia ya Filamu na Muziki

Mamlaka ya mapato (TRA) kurasimisha kazi zaTasnia ya Filamu na Muziki


 

Afisa Utafiti Mwandamizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bwana Emphraim Mdee akiongea na Wanahabari (hawapo pichani) kuhusu Urasimishaji wa Tasnia ya Filamu na Muziki Tanzania na kuanzishwa kwa utaratibu wa kubandika stempu za kodi kwenye kazi za wasanii,katikati ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu Tanzania Bibi Joyce Fissoo.(Picha na Benjamin Sawe wa WHVUM).
 ……………………………………………………………..
Na Heka Wanna na Shakila Galus-MAELEZO_ Dar es salaam

 Serikali imeeleza kuwa kuanzia Januari mosi mwakani (2013) itaanza kubandika stempu za kodi katika bidhaa za filamu na muziki.
 Hatua hiyo inalenga  kuwasaidia wasanii wa filamu na muziki kupata mapato ya kazi zao na kuweka mfumo mzuri wa namna ya kudhibiti wizi wa kazi zao kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania
 Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Utafiti Mwandamizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Ephraim Mdee alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam.
 Alisema kuwa TRA kwa kushirikiana na wadau wengine wataanza kubandika stempu za kodi(Tax Stamps)ambazo zitakuwa  maalum ili kusaidia usimamizi na udhibiti wa kazi za wasanii ambazo zitawekwa katika DVD, CD, na Tape.
 Mdee aliongeza kuwa kazi za wasanii ambazo tayari ziko sokoni zitakiwa zirudishwe kwa ajili ya kubandikwa stempu na kuongeza kuwa zoezi la kurudishwa litafikia ukomo Mwezi Julai mwakani.
 Alisema kuwa baada ya hapo mtu atakayekutwa akiuza kazi ambazo hazina stempu ya kodi atachukuliwa hatua ya kuvunja sheria.
 Hivyo ametoa wito kwa wasambazaji wote kukusanya kazi ambazo wamezipeleka sehemu mbalimbali kabla ya Julai mwakani .
 Aidha alisema kuwa TRA pia itanzishwa mfumo wa pamoja wa kieletroniki wa mawasiliano ambao utaunganisha taasisi zote zinazo husika na tasnia ya filamu na muziki ili kuhakikisha kuwa taarifa za wadau au wasanii zinapatikana kwa uhakika na usahihi
 Alitoa kwa wananchi wote kuhakikisha kuwa wanashiriki  katika kulinda,kuthamini na kuendeleza tasnia za filamu na muziki kwa kununua bidhaa zilizowekwa stempu za kodi
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger