Pages

Home » » SERIKALI KUWAKAMATA WALIOANZISHA VIWANDA BUBU VINAVYOZALISHA BIDHAA CHINI YA KIWANGO

SERIKALI KUWAKAMATA WALIOANZISHA VIWANDA BUBU VINAVYOZALISHA BIDHAA CHINI YA KIWANGO

 
 
NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu, amesema serikali kuanzia sasa itawakamata  baadhi ya watu waliyojianzishia viwanda bubu vinavyozalisha bidhaa hafifu nchini.
 
Kauli hiyo ilitolewa, na waziri huyo  wakati alipotembelea viwanda vinavyomilikiwa na Kampuni ya MMI Steel Mills Limited vilivyoko Mikocheni jijini Dar es Salaam jana.
 
Alisema lengo la kuwakamata watu hao ambao wamo hata wageni                                                                                                                                  , na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria ni kudhibiti bidhaa hizo kwenye soko ambapo zimekuwa zikiwatia hasara wananchi pia kuviharibia sifa baadhi ya viwanda.
 
Teu alisema viwanda hivyo vimekuwa vikiiga bidhaa kama nondo na mbati, kutumia nembo za kampuni mbalimbali zinazotambulika nchini kama vile MMI Steel Mills Limited.
 
Alisema kutokana na ubabaishaji huo unaofanywa na baadhi ya watu, serikali itahakikisha inazisaidia kampuni zote zilizoanzishwa kwa kufuata sheria.
 
“Kampuni hii ya MMI Steel Mills imekuwa kwa muda mrefu ikitoa mchango mkubwa katika kuchangia pato la taifa haswa kwenye eneo la kodi pia imepanua wigo wa ajira kwa Watanzania ambapo pia kimekuwa kikiingizia Tanesco jumla ya sh. bilioni 1 kama bili kwa mwezi  ”alisema Teu.
 
Akizungumzia kuingiliana kwa mipaka kati ya Kiwanda hicho na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC katika mradi wa kutengeneza chuma cha Liganga na mkaa wa mawe huko Katewaka, Teu alisema, hata yeye utata huo umemshtua sana.
 
Alisema matatizo hayo yamesababishwa utoaji wa zabuni, kutokana na upande mmoja kutokuwa makini ambapo pia aliwaomba wasichoke, watalifanyia kazi kama wizara.
 
Awali Mhandisi, Raulence Manyama viwanda hivyo vya chuma, vilikuwa vikikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa chuma.
 
Alisema hadi kufikia mwa 2012 kulikuwa na viwanda na viwanda 21 vya chuma nchini vyenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 200,000 za chuma kwa mwaka.
 Aliasa serikali kuongeza uwezo   nchi kuzalisha aina nyingi ya bidhaa ya chuma ambazo kwa sasa zinatoka nchi za nje, hizo ni hot-roll coils, cold coils, flat bars na aina nyingi za chuma.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger