Pages

Home » » HII NDIYO SHULE WALIYOSOMA VIONGOZI NA WASANII WAKUBWA "IMETELEKEZWA"

HII NDIYO SHULE WALIYOSOMA VIONGOZI NA WASANII WAKUBWA "IMETELEKEZWA"


Jengo la shule ya sekondari ya Ufundi Ifunda iliyopo katika Wilaya ya Iringa, "Ifunda Technical Secondary School". Ambayo imesomwa na viongozi wengi wakubwa nchini, na wasanii wenye majina makubwa ndani na nje ya nchi.
Wanafunzi wakiwa nje ya shule yao
 Majengo haya kama yangefanyiwa japo UKARABATI yangeweza kupendeza na hivyo kuvutia uwekezaji wa elimu kwa vijana nchini na hata nje ya nchi, kwani shule hii ni maarufu na pia niya wanafunzi wenye VIPAJI.
 Jengo hili ni kama nembo "Logo" ya shule ya sekondari ya Ufundi Ifunda, Limechoka, siku ya kushindwa kuvumilia uchakavu huu wanafunzi wanaweza kupata madhara makubwa, kwani jengo hili sasa ni chakavu mno.
Enzi hizoooo!! Hili lilikuwa ni Bus kwa ajili ya kuwasafirisha wanafunzi, yaani ulikuwa ni usafiuri wa shule, jamani leo hii lipo "Hoi bin taabani", Imebaki stori.
 Magari haya nayo yalitumiaka kusafirisha wanafunzi pamoja na kufanya shughuli mbalimbali za shule ya sekondari ya ufundi Ifunda. Jamaaanii!!
 Haya nayo nimajengo au tuyaite madarasa katika shule yaa Ufundi Ifunda, enzi zake yalikuwa mazuri, sasa kutokana na kukosa ukarabati yamezeeka.
 Makamu mkuu wa shule ya sekondari Ufundi Ifunda Bw. Shabani Nsute akisoma risala ya shule yake mbele ya ugeni katika mahafali ya 12 ya kidato cha sita cha wanafunzi wa sekondari ya Ufundi Ifunda Iringa.
 Mmhhhh!!
 Wanafunzi wahitimu wa elimu ya kidato cha sita sekondari ya Ufundi Ifunda wakisikiliza jambo katika mahafali yao.
 Hiki ni choo, kwa wakati huo kilikuwa nicha kisasa sana, kweli enzi hizo uwekezaji katika elimu ulifanyika kwa kiwango kikubwa, shule kuwa na zaidi ya magari matano kwa ajili ya wanafunzi na shughuli za shule siyo jambo la kitoto, leo hii magari yote hayafai, na hivyo shule kutokuwa na gari hata moja la shule.

HABARI KAMILI

WALIMU na wanafunzi wa sekondari ya ufundi Ifunda iliyopo katika Wilaya ya Iringa wameulalamikia uongozi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kwa kushindwa kukarabati shule hiyo ambayo ni moja ya shule kongwe hapa nchini.
Hayo yalizungumzwa na walimu na wanafunzi hao katika mahafali ya 12 ya kidato cha sita na kuwa shule hiyo majengo yake yamechaka na hivyo kupunguza ari ya wanafunmzi kupenda masomo.
Walisema shule hiyo imechakaa miundombinu yake mingi kama umeme, maji pamoja na majengo yake yakionekjana kama magofu, kutokana na kjuwa na umri mkubwa tangu tangu ianze kutumika mwaka 1950 kabla nchi hii haijapata Uhuru.
Esther Mhode mwanafunzi wa shule hiyo yaUfundi  Ifunda, alisema majengo yake yanakatisha tamaa  kuendelea na masomo, kwani miundombinu ni mibovu hasa majengo ambayo ndiyo kivutio kikubwa kwa wanafunzio kupenda masomo.
“Kama unavyoona majengo yetu utadhani ni magofu, au majengo ya kumbukumbu, hali hii kwa kweli inachangia sana kushusha hata kiwango cha ufaului waetu, kwani shule haina mvuto wa mwanafunzi kupenda kujisomea, majengo nayo ni chachu kubwa katika kuboresha elimu, huwezi kuamini hapa tunaambiwa wamesoma viongozi wakubwa na wasanii maarufu, lakini hawana mchango wowote katika shule,”
Geofrey Nyamasagi muhitimu wa kidato cha sita shuleni hapo, alisema endapo serikali ingeboresha majengo ya shule hiyo, ingekuwa ni mfano wa kuigwa hasa kwa kuwa shule ni moja ya shule kongwe hapa nchini.
“Humu ndani kuna mitambo ya ufundi imechakaa, inaelekea zamani wanafunzi waliosoma katika shule hii walipata elimu sahihi, na ndiyo maana wengi wao ni viongozi wa ngazi za juu ndani na je ya nchi,  shule niya vipaji malumu, lakini sasa kwa kweli imesahaulika mno, serikali pamoja na wadau wa elimu hasa waliosoma katika shule hii wangefanyia matengenezo ili kuifanya iwe endelevu,”
Wanafunzi hao walisema licha ya changamoto hiyo ya miundombinu pia kuna uhaba wa walimu, hasa wa masomo ya ufundi, Sayansi na Hisabati na hivyo kushindwa kupata elimu sahihi waliyokusudia, huku changamoto nyingine kama upungufu wa vifa vya kujifunzia hasa kw masomo ya Ufundi na Sayansi.
Naye makamu mkuu wa shule hiyo Shabani Nsute alisema changamoto ya miundombinu ya maji inasababisha wanafunzi kutumia muda mwingi kuacha masomo na kwenda kuchota maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya shule.
Nsute alisema uchakavu wa miundombinu ya shule husababisha wanafunzi kuacha masomo na kwenda kuchota maji ya kupikia na matumizi ya vyoo ambavyo vilijengwa kwa mfumo wa matumizi ya maji mengi.
Alisema hata nyumba zao walimu ni chakavu licha ya shule hizo kulipa kodi, lakini hazijawahi kufanyiwa ukarabati wa aina yoyote kwani na kuwa  awali ilianza kama chuo cha ufundi (Ifunda Trade School) mwaka 1950 na mwaka 1964 chuo kilibadilishwa na kuwa shule ya sekondari ya ufundi.
Ofisa elimu taaluma sekondari Wilaya ya Iringa Devotha Luwungo alisema ili kukabiliana na changamoto za shule hiyo, serikali imeanza kutoa shilingi Miliono hamsini kwa ajili ya kukarabati miundombinu ya shule kongwe, na sasa fedha hizo zitaelekezwa katika shule hiyo.
Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Patric Golwike alisema ofisi yake imetoa shilingi Milioni 5 fedha kwa ajili ya kununulia mifuko 30 ya Saruji ili kuanza ukarabati katika nyumba za walimu wa shule hiyo ya Ufundi Ifunda.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger