Pages

Home » » ZFA Yawafungia Wachezaji Wake Wote wa Timu ya Taifa

ZFA Yawafungia Wachezaji Wake Wote wa Timu ya Taifa


 
Baadhi ya wachezaji wanaounda kikosi cha Zanzibar Heroes

CHAMA cha Soka Zanzibar (ZFA) kimewafungia wachezaji wake wote waliokuwa katika kikosi cha timu ya taifa (Zanzibar Heroes) ambao walikuwa wakishiriki michuano ya CECAFA Tusker Chalenji. Wachezaji hao wamefungiwa kucheza soka ndani na nje ya nchi na kutakiwa kurejesha fedha zote za zawadi ya Dola 10000 za msindi wa tatu walizopokea nchini Uganda na kuamua kugawana wenyewe bila kushirikisha uongozi.

Kwa mujibu wa taarifa ya ZFA waliofungiwa ni:- makipa; Mwadini Ali (Azam), Suleiman Hamad (Black Sella), Abdalla Juma (Kipanga), mabeki; Nassor Masoud ‘Chollo’ (Simba), Samir Haji Nuhu (Azam), Aggrey Morris (Azam), Nadir Haroub Ali ‘Canavaro’ (Yanga), Aziz Said Ali (Kmkm), Mohammed Juma Azan (JKU) na Ali Mohammed Seif (Mtende Rangers).

Wengine ni viungo; Hamad Mshamata (Chuoni), Ali Bakar (Mtende Rangers), Is-haka Mohammed (JKU), Twaha Mohammed(Mtibwa Sugar), Suleiman Kassim ‘Selembe’ (Coastal Union), Saad Ali Makame (Zanzibar All Stars), Makame Gozi (Zimamoto), Issa Othman Ali (Miembeni), Aleyuu Saleh (Black Sella), Khamis Mcha Khamis ‘Viali’ (Azam) na washambuliaji; Amir Hamad (JKT Oljoro), Jaku Juma Jaku (Mafunzo), Abdallah Othman (Jamhuri), Nassor Juma (JKU) na Faki Mwalim (Chipukizi).

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger