Pages

Home » » MADIWANI WALIA NA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UCHUMI.

MADIWANI WALIA NA VIONGOZI WANAOKWAMISHA UCHUMI.


 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Bw. Steven Mhapa akisikiliza hoja za madiwani.
 Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bw. Patric Golwike akiwasikiliza madiwani wa Halmashauri yake.
 Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Bi. Ritha Mlagala akiwa katika kikao hicho cha baraza la madiwani.
 Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wakiwa katika baraza lao.

Tunasikiliza kwa makini" Niwa baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wakiwa katika baraza la madiwani.

Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wakisikiliza kikao cha baraza la madiwani.
IMEFAHAMIKA kuwa changamoto kubwa inayodumaza uchumi katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ni pamoja na viongozi kukwepa kulipa ushuru wa biashara,  pamoja na baadhi ya mawakala kuiba fedha katika vituo vya ushuru.
Hayo yamezungumzwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, katika kikao cha baraza la madiwani mabapo amesema viongozi  wa aina hiyo wanavunja  sheria za ulipaji kodi, kwa kutumia wadhfa walionao.
Aidha Mhapa amesema baadhi ya vituo vya mawakala ni kitovu cha wizi wa fedha za ushuru, na hivyo kuwataka wataalamu wa Halmashauri kupanga mkakati wa namna ya kudhibiti hali hiyo, pamoja na njia sahihi za kubinafsisha ukushanyaji wa ushuru, ili kuwasaidia wananchi kwa  kurudisha asilimia 20 ya  vijiji vinavyotoa mazao hayo.
Aidha madiwani hao wameitaka serikali kuyahimiza mashirika na asas za kiraia zinazojihusisha na ugawaji wa mipira ya kiume (Kondomu) kuzigawa pia na kondomu za kike ili kuwawezesha wanawake kuwa na uhuru wa matumizi ya dhana hizo.
Bi. Vumilia Mwenda diwani wa tarafa ya Kiponzelo/Ifunda,  amesema ubaguzi unaofanywa katika  kuzigawa kondomu hizo unawanyima haki wanawake kuwa na maamuzi ya kutumia zana hizo.
Naye Bi.  Ameria Galinoma diwani wa Kata ya Kalenga amesema kuna haja kondomu hizo zote zikawekwa katika vyoo vyote vya nyumba za starehe, kwani baadhi ya wananchi wanaona aibu kununua madukani.
Hata hivyo mratibu wa ukimwi Wilaya ya Iringa  Odia Hezron amesema kondomu za kike hazipatikani kwa urahisi, na kuwa hata utumiaji wake ni mgumu, ambapo wanawake wengi hawazipendi Kondomu hizo.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger