Pages

Home » » Bwawa Lililogharimu Sh 47 Milioni Lashindwa Kutumika

Bwawa Lililogharimu Sh 47 Milioni Lashindwa Kutumika

• LILITAKIWA KUMWAGILIA EKARI 400, SASA LAHITAJI MAMILIONI MENGINE 
Na Daniel Mbega 
MIAKA minne iliyopita, yaani mwaka 2009, wakati ujenzi wa Bwawa la Maji katika Kijiji cha Magulilwa wilayani Iringa unakamilika, wananchi wa kijiji hicho na Kata yote ya Magulilwa waliamini walikuwa wamekombolewa. 
Hiyo ilitokana na ukweli kwamba, mradi huo ungetosheleza kilimo cha umwagiliaji cha hekta 400 pamoja na huduma nyingine za kijamii likiwemo josho la kuogeshea mifugo kijijini hapo. 
Hata hivyo, kwa miaka minne sasa, ndoto hizo zimeyeyuka kwani bwawa hilo limeshindwa kufanya kazi baada ya kujengwa chini ya kiwango licha ya kugharimu Sh 47 milioni, fedha ambazo zilitoka kwenye Mradi Shirikishi wa Maendeleo ya Kilimo na Uwezeshaji (PADEP – Participatory Agricultural Development and Empowerment Project), Halmashauri ya Wilaya pamoja na nguvu ya wananchi. 
Mradi wa bwawa hilo ndio uliokuwa pekee kwa Mkoa wa Iringa kati ya miradi 69 ya malambo na visima iliyofadhiliwa na Padep nchi nzima tangu mwaka 2004 ambapo hadi mwaka 2007 yalikuwa yamegharimu jumla ya Sh 3,003,785,439. 
Mikoa mingine na idadi ya malambo ikiwa kwenye mabano ni Arusha (5), Kilimanjaro (1), Manyara (28), Tabora (2) na Singida (32). 
“Usimamizi mbovu ndio uliofanya bwawa hili lijengwe kienyeji na chini ya kiwango licha ya kutumia fedha nyingi, lakini hili ndilo lingekuwa mkombozi mkubwa wa wananchi wa Magulilwa kiuchumi kwa sababu kuna eneo kubwa la bonde kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji,” anasema Ernest Kasike, Diwani wa Kata ya Magulilwa.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger