Pages

Home » » TAHLISO WAPINGA MAANDAMANO YALIYOPANGWA KUFANYIKA KESHO IJUMAA

TAHLISO WAPINGA MAANDAMANO YALIYOPANGWA KUFANYIKA KESHO IJUMAA

DSC_4824 
Makamu Mwenyekiti wa TAHLISO Abdi Mahmoud Abdi akizungumza na Waandishi wa habari leo Mjini Idara ya Habari maelezo Zanzibar kuhusu kukanusha Taarifa ya Maandamano yaliyopangwa kufanyika hapo kesho. Picha na Makame Mshenga

Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar 14/08/2014
Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu TAHLISO limekanusha Taarifa zilizosambazwa katika Vyombo vya habari na Mitandao ya Kijamii juu ya kuwepo wa maandamano ya Wanafunzi wa Vyuo vikuu yanayotarajiwa kufanyika hapo kesho Ijumaa.
Shirikisho hilo pia limesema Taarifa za kuwepo kwa maandamano hayo hazijatolewa na TAHLISO na kuwaomba Wanafunzi kutojaribu kushiriki katika Maandamano hayo.
Akizungumza na Waandishi wa habari leo Mjini Zanzibar Makamu Mwenyekiti wa TAHLISO Abdi Mahmoud Abdi amesema aliyesambaza Taarifa za Maandamano hayo ni Mtu ambaye alishavuliwa Nyadhifa za Uongozi wa TAHLISO na kwamba anachokifanya ni Upotoshaji na kujipalilia kisiasa.
“Anayejiita Mwenyekiti wa TAHLISO Musa Mdede SI MWENYEKITI HALALI kwasababu vikao halali vya Shirikisho vilivyofanyika May 3,4,2014 katika Chuo cha kodi vilimwondoa madarakani na kwa mujibu wa Katiba nafasi yake ilikaimiwa na Makamu wake ” Alisema Abdi
Amesema sababu ya Msingi ya kumuondoa katika nafasi yake ilitokana na kwenda kinyume na Katiba kwa kujiingiza katika Siasa ambapo aligombea na kuangushwa katika kura za maoni kupitia CHADEMA.
Amedai kuwa anachokifanya Mdede kwa sasa ni upotoshaji kwa TAHLISO ambapo anajitangaza kwa malengo ya kugombea uchaguzi mkuu unaokuja wa mwaka 2015.
Amefahamisha kuwa licha ya kuwepo na Taarifa ya Baadhi ya Vyuo kutokupata Pesa kwa ajili ya Mafunzo ya Vitendo TAHLISO imekuwa bega kwa bega kuhakikisha suala hilo linapatiwa majibu ya haraka.
Amesema BODI ya Mikopo inaendelea kuchukua hatua za haraka katika kuhakikisha Vyuo husika Vinapatiwa fedha na kwamba siku ya Leo Bodi itatoa Fedha kwa Chuo kikuu Kishiriki  cha kumbukumbu ya Stephano Moshi (SMUCCO)  na Chuo kikuu cha Jordan Morogoro.
“Chuoni siyo sehemu ya kufanya Siasa bali ni sehemu ya kusoma, Maandamano siyo suluhu njia pekee ni mazungumzo na tunaendelea kuyafanya” Alifafanua Abdi.
Aidha Makamu Abdi amesema taratibu zinazohitajika zinaendelea kuchukuliwa ili Vyuo vingine vilivyobakia viweze kupata fedha hizo.
Vyuo ambavyo havijapata Fedha za Mafunzo kwa Vitendo ni pamoja na Chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino(SAUT) Mwanza na Tabora, Chuo cha Usimamizi wa Fedha(IFM), Chuo kikuu cha Teofilo Kisanji Mbeya na Chuo kikuu cha Tumaini Makumira-Iringa.
Katika taarifa zilizosambaa kwenye Vyombo vya habari na Mitandao ya kijamii inadaiwa kesho Ijumaa kutafanyika Maandamano ya amani ya Wanafunzi wa Vyuo vikuu kuelekea Ofisi za Waziri Mkuu kushinikiza Serikali kutoa Shiligi Bilioni 6.6 kwa ajili ya mafunzo ya Vitendo kwa wanafunzi hao.
Makamu huyo ambaye anashika nafasi ya Uenyekiti kwa sasa amewaomba Wanafunzi ambao hawajapata fedha zao kuwa watulivu wakati wakisubiri kupata fedha zao huku hatua za haraka zikichukuliwa.
IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger