Pages

Home » » MBUNGE WA ARUSHA KUPITIA CHADEMA ASEMA KINANA AMEDANGANYWA NA WANACCM WENZAKE

MBUNGE WA ARUSHA KUPITIA CHADEMA ASEMA KINANA AMEDANGANYWA NA WANACCM WENZAKE


Siku moja baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuwapokea viongozi wawili akisema wanatoka Chadema na kumtuhumu Mbunge wa Arusha, Godbless Lema kuwa anatumia madaraka yake kujinufaisha na mali za umma, mbunge huyo amejibu akisema: “Kinana amepigwa changa la macho.”


Akiwa Arusha mwishoni mwa wiki Kinana aliwapokea waliokuwa wenyeviti wa Chadema katika Wilaya ya Monduli, Amani Silanga na wa Ngorongoro, Revocatus Palapala lakini jana Lema alisema viongozi hao walikwishatimuliwa Chadema tangu mwaka 2013.

Kinana alisema migogoro ya CCM ndiyo iliyokinufaisha Chadema na Lema akaingia madarakani, lakini akawataka wananchi kujutia uamuzi huo na kutorudia kumchagua mbunge huyo.

“Mbunge wenu ameshindwa kutekeleza kile mlichomtuma bungeni badala yake anatumia madaraka yake kujimilikisha mali za umma na kutukana hovyo,” alisema na kuongeza:


“Mfano ni lile shamba alilopewa na Mayala ambalo ameliuza, trekta na vifaa vingine vyote ameviuza lakini migogoro ya ardhi na maji ameshindwa kuitatua.”

Majibu ya Lema

Akijibu tuhuma hizo, Lema alisema Kinana amepigwa ‘changa la macho’ na amefanyiwa maigizo kama ya futuhi na watu wa usalama wameshindwa kumwambia ukweli.


Alisema mambo yote aliyoambiwa ni uongo mtupu ambao yeye hawezi kusumbuka nao.


“Kama mimi ni mwizi na tapeli, hivi hata usalama wanashindwa kuwaeleza ukweli washughulike na mimi? Ndiyo maana watu tuliowafukuza Chadema wamewapokea eti wamehama chama. Wameingizwa mjini hao,” alisema.


Alisema: “Silanga na Palapala walifukuzwa tangu Novemba 30, 2013 baada ya kubainika kuwa kwenye mtandao wa Zitto na wote walitimkia ACT kama walivyofanya kina Mwigamba (Samson) na Kitila Mkumbo,” alisema Lema akitoa nakala ya taarifa kwa vyombo vya habari.

Alisema baadaye Silanga na Palapala walijiunga CCM na Palapala aligombea na kushinda uenyekiti wa Kijiji cha Wasso wilayani Ngorongoro kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa Desemba 14, mwaka jana.

“Ni maajabu ya mwaka mwenyekiti wa kijiji kupitia CCM tangu Desemba 14, mwaja jana, apokewe na Kinana akitangazwa kukihama Chadema?” alisema Lema.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger