Hakimu wa
mahakama ya mwanzo Mwanjelwa JP MWAMBAPA ameitaka jamii kutumia mabaraza ya
kata na mitaa katika kusuhisha kesi za kifamilia na madai ili kutoa nafasi kwa
mahakama kusikiliza kesi ambazo zimekuwa vigumu kuamriwa na mabaraza hayo.
Aliyasema
hayo wakati wa mahojiano na mtandao huu ofisini kwake na kudai kuwa kesi nyingi
zimekuwa zikishindwa kufikiwa muafaka kutokana na wanafamilia wenyewe kushindwa
kuyatumia mabaraza ya kata.
Aidha
MWAMBAPA alizitaja baadhi ya kesi zinazoongoza kusikilizwa mahakamani hapo kuwa ni kesi
za mirathi, talaka na madai ambapo kwa sehemu kubwa zimekuwa ni vigumu kutolewa
hukumu kutokana na walalamikaji kutopitia kwenye mabaraza ya kata pamoja na
vyombo vya dini.
Hata hivyo
alisema chanzo cha kesi hizo ni mmomonyoko wa madili ndani ya jamii.
1 comments:
Itasaidia kupunguza kwa mrundikano wa kesi mahakamani na kusikilizwa kwa wakati muafaka na kuepusha rushwa!!
Post a Comment