Watu
wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti akiwemo MAGRETH MWAKASEGE
mwenye umri wa miaka 36 aliyefariki dunia kwa kuungua moto na kusababisha
majeruhi kwa mtu mmoja wakati wakiwa wamelala nyumbani kwao.
Akiongelea
matukio hayo Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya BARAKIEL MASAKI alisema
tukio hilo
limetokea jana majira ya saa tano za usiku kata ya Ilemi mtaa wa Mapelele na
kusema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha moto huo ni hitilafu ya
umeme.
Aidha alimtaja
aliyejeruhiwa kuwa ni MAWAZO MWAKASEGE mwenye umri wa miaka 39 ambaye ni mume
wa marehemu na yupo katika hospitali ya rufaa kwa ajali ya matibabu
Wakati
huohuo kamanda MASAKI alisema watu wasiofahamika wamevunja kanisa la UYOLE
CHRISTIAN FELLOWSHIP na kuiba vitu vyenye thamani ya shilingi million 8 majira
ya saa tano na dakika 20 usiku maeneo ya uyole mtaa wa sokoni.
Aliongeza kuwa jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa kuwabaini waliohusika na tukio hilo la wizi na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano na Jeshi la polisi ili kufanikisha kuwatia mbaroni watuhumiwa hao.
0 comments:
Post a Comment