Pages

Home » » VITA VYA WENYEWE KWA WENYEWE NCHINI SOMALI HUENDA VIKAMALIZIKA KAMA SERIKALI YA NCHI HIYO ITAKAMILISHA ADHIMA YAKE KUKABIDHI MADARAKA KESHO

VITA VYA WENYEWE KWA WENYEWE NCHINI SOMALI HUENDA VIKAMALIZIKA KAMA SERIKALI YA NCHI HIYO ITAKAMILISHA ADHIMA YAKE KUKABIDHI MADARAKA KESHO

Serikali ya mpito ya Somalia itakabidhi madaraka kesho kwa serikali ya kudumu baada ya kuongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 8. Bunge la Somalia linatazamiwa kuchagua rais mpya wa nchi hiyo kesho na kukabidhi madaraka ya nchi kwa serikali ya kudumu. Habari zinasema serikali ya mpito ya Somalia mbayo imekuwa madarakani tangu mwaka 2004 itajiuzulu kesho na kukabidhi madaraka kwa serikali mpya. Serikali hiyo ya mpito inakosolewa kwamba haikuweza kurejesha amani kamili nchini Somalia katika kipindi cha miaka 8 iliyopita. Rais wa serikali ya mpito inayomaliza muda wake Sheikh Sharif Sheikh Ahmad, Waziri wake Mkuu Abdiweli Muhammad Ali na Spika wa Bunge la Somalia Sharif Hassan Sheikh Adam wanagombea kiti cha rais katika uchaguzi wa kwanza wa kisiasa wa Somalia tangu miaka 20 iliyopita.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Greyson Salufu | Chimbuko Letu Inc | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Mbwile Media - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger